Search This Blog

Tuesday, July 27, 2021

Waziri Mkuu wa zamani apewa jukumu la kuunda serikali mpya Lebanon


Rais wa Lebanon Michel Aoun alimpa jukumu la kuunda serikali mpya Waziri Mkuu wa zamani Najib Mikati baada ya kiongozi wa cham cha Future Movement Saad al-Hariri.

Rais Aoun alikamilisha mikutano ya mashauriano na vikundi vya kisiasa katika Bunge kuamua jina ambalo litachukua nafasi ya serikali ya Hassan Diyab, ambaye alijiuzulu mnamo Agosti 10, 2020, kufuatia maandamano dhidi ya mlipuko uliozuka katika Bandari ya Beirut.

Katika taarifa ya maandishi iliyotolewa na Ofisi ya Rais baada ya mazungumzo hayo, ilielezwa kuwa Mikati aliitwa katika Ikulu ya Baabda ili kupewa jukumu la kuunda serikali mpya.

Mfanyabiashara na naibu Mikati, ambaye aliwahi kuwa waziri mkuu nchini Lebanon kati ya mwaka 2005 na 2011, alipokea kura za wanachama 72 kati ya washiriki 115 waliohudhuria mikutano hiyo katika ikulu ya Rais ya Baabda.

Mikati alitangaza katika mkutano na waandishi wa habari baada ya kukutana na Rais Aoun kwamba alipewa jukumu la kuunda serikali mpya.

Akieleza kuwa hataweza kushinda shida peke yake na kwamba alidai uaminifu kutoka kwa umma, Mikati alisema wataunda serikali mpya kwa kushirikiana na Rais wa Ufaransa, kulingana na mpango wa Ufaransa.

Lebanon, ambayo ina muundo dhaifu sana kwa upande wa mgawanyiko wa kisiasa kulingana na dini na madhehebu tofauti, inakabiliwa na shida kubwa ya kiuchumi tangu vita vya wenyewe kwa wenyewe vya 1975-1990.

Mlipuko mkubwa katika Bandari ya Beirut uliotokea mnamo Agosti 2020 ulizidisha shida za kiuchumi nchini Lebanon na kusababisha mzozo mpya wa serikali.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...