Search This Blog

Sunday, July 4, 2021

Waziri Kalemani atoa mwezi mmoja kwa shirika la TPDC kuanza utekelezaji wa ujenzi wa mradi wa bomba la mafuta

Waziri wa Nishati Medard Kalemani ametoa mwezi moja  Shirika la maendeleo la petrol nchini TPDC kuanza utekelezaji wa ujenzi wa Mradi wa Bomba la mafuta ghafi kutoka nchi Uganda hadi Chongoleani Jijini Tanga.

Rai hiyo alilitoa leo wakati wa kikao kazi  cha maandalizi ya utekelezaji wa Mradi wa ujenzi wa Bomba la mafuta kilichofanyika Jijini Tanga alisema kuwa muda wa vikao kwa ajili ya majadiliano umekwishwa na kinachotakiwa kwa sasa kuanza utekelezaji wake.

Alisema kuwa sekta binafsi ipo tayari kwa ajili ya kuchangamkia fursa za ujenzi hivyo aliitaka TPDC kuanza maandalizi ya ujenzi wa Mradi huo ili kutoa fursa kwa wananchi kuweza kupata ajira na hivyo kuinua uchumi wao.

“Niwaombe TPDC hii iwe mkutano wa mwisho tunataka kuja kuitwa kwenye vikao vya kujadili namna ambavyo kazi zimefanyika kwani sasa wananchi wanataka kuona namna ambavyo wanashiriki katika Mradi huo” alisema Waziri Kalemani.

Alisema kuwa kuwa Mradi huo unatarajiwa kuwekeza zaidi ya sh Tril 8.4 ambazo lengo la Serikali ni kuhakikisha fursa hiyo ya uwekezaji inawanufaisha sekta binafsi ili kuongeza wingo wa kiuchumi.

Waziri Kalemani alisema wakati wa kazi za ufundi na nyengine kwenye haya matenki na hakuna sehemu nyengine itajengwa mradi huo tofauti na hapa Tanga hiyo itachukua ajira za hapa hapa nchini hatarajii watoke nje ya nchi.

Alisema katika utekelezaji wa mradi huo watanzania wengi wataajiriwaa na itachukua wafanyakazi wengi sana hivyo watanzania wengi wahakikishe wanajipanga kuchangamkia fursa zitakazokuwepo.

“Nitoe tamko kwamba watanzania wanaweza hata mabomba yatakayojenga mradi huo serikali kupitia Rais Samia Suluhu wanataka yaweza kutoka hapa nchini kama ni muda wa kujipanga na kujiandaa muanze leo haiwezi kuingia akilini mabomba ya kupikia mafuta yatokea nje maana yake manufaa yanaendelea kupungua”Alisema

Waziri huyo aitoa rai kwa watanzania wengi uwezo kuchangamkia fursa za mikopo kwenye mabenki  kupata fedha waweze kujenga viwanda vya mabomba hapa nchini hayo ndio manufaa tunayoyataka .

“Hivyo fursa hii watanzania tuiifumbie macho…Agizo langu Kampuni itakayojenga mradi huo wakandarasi mtakaowapa kazi mhakikishe vifaa ujenzi vinatoka hapa nchini”Alisema

Hata hivyo alisema suala la pili manufaa makubwa yatatokana na ajira watanzania wasiopungua efu 15,000 wataajiriwa kwenye mradi huo hivyo mjiandae kuchangamkia fursa hizo.


Awali akizungumza katika semina hiyo Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Dkt James Matarajio alisema kikao hicho lengo lake ni kuweza kukutana kuweza kushirikishana habari za mradi wa (EACOP) wamefikia wapi na wanaendelea wapi na fursa zilizopo.

Alisema Shirika hilo ni Taasisi ambayo inaweza kusimamia mradi huo na kuhakikisha unasimamia maslahi mapama ya Taifa yanatekelezwa na kulindwa ili kuweza kuleta tija kubwa .

Mkurugenzi huyo alisema EACOP ni moja ya miradi 16 ambayo ni ya kielelezo kama utakumbuka wiki iliyopita Waziri Mkuu alizindua mpango wa tatu wa maendeleo ya miaka mitano katika huo mpango na hiyo mradi huo ni miongoni mwao.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...