Wafuasi vijana wa chama cha mabadiliko ya kidemokrasia(Congress for Democratic Change ) nchini Liberia wamepata hasira baada ya waziri mdogo katika ofisi ya rais kuonekana katika video akiwa anamzawadia mke wake gari la gharama huku akilimwagia shampeni.
Tukio hilo liliripotiwa kuwa sherehe ya kuzaliwa kwa mke wake.
Chama hicho cha vijana kimeelezea kitendo alichokifanya James Emmanuel Potter wiki iliyopita ni cha kizembe kwa kuonesha utajiri aliokuwa nao.
Wamesema jambo kama lile linakanganya na kwenda tofauti na kanuni na itikadi za kuanzishwa kwa chama chake.
Wafuasi hao wanamshutumu ofisa huyo ambaye ni msimamizi wa vifaa katika ofisi ya urais - kwa kutojali uhalisi wa wakati huo, katika moja ya nchi masikini zaidi Afrika.
Lakini msaidizi huyo wa waziri alijibu baada ya kukosolewa na kuandika katika Facebook kuwa anafanya kazi ili kupata mshahara wa kumuwezesha kupata chochote kitakachompendeza.
Hii ni video iliyowekwa Facebook ikimuonesha waziri mdogo huyo akimzawadia mke wake gari :
Mtumiaji mmoja wa wa Facebook alimkosoa naibu waziri kwa kusema kitendo cha bwana Potter,kumnunulia mke wake Audi SUV na kumwaga shampeni ya gharama wakati wananchi wanaangaik na maisha. Je huyu ni maskini?"
"Sababu moja kuwa maskini kwasababu ya ajira za serikali. Wanaishi maisha ya kifahari kwa gharama za watu maskini kuhangaika!" mtu mwingine aliandika.
Wakati wengine walimtetea afisa huyo, akisema hakuna tatizo kwa mume kumnunulia mke wake gari . Anafanya kazi na naamini kipato chake kinamwezesha kununua gari hili dogo, acheni chuki".

No comments:
Post a Comment