Katika operesheni dhidi ya shirika la kigaidi la Boko Haram kaskazini mashariki mwa Nigeria, wanamgambo 37 wa shirika hilo waliangamizwa.
Msemaji wa Jeshi la Anga la Nigeria (NAF) Edward Gabkwet alitangaza kwamba wanajeshi walifanya operesheni ya angani na ardhini dhidi ya Boko Haram katika mkoa wa Bula wa jimbo la Yobe.
Wakati wanamgambo 37 wa Boko Haram wakiuawa katika operesheni hiyo, magaidi wengi walitoroka wakiwa na majeraha.
Akieleza kuwa makaazi ya magaidi yaliharibiwa kwenye operesheni hiyo, Gabkwet alitangaza kwamba risasi na silaha muhimu zinazomilikiwa magaidi pia zilikamatwa.

No comments:
Post a Comment