Search This Blog

Sunday, July 4, 2021

Wanamgambo 37 wa Boko Haram waangamizwa kwenye operesheni iliyoendeshwa na jeshi la Nigeria

Katika operesheni dhidi ya shirika la kigaidi la Boko Haram kaskazini mashariki mwa Nigeria, wanamgambo 37 wa shirika hilo waliangamizwa.

Msemaji wa Jeshi la Anga la Nigeria (NAF) Edward Gabkwet alitangaza kwamba wanajeshi walifanya operesheni ya angani na ardhini dhidi ya Boko Haram katika mkoa wa Bula wa jimbo la Yobe.

Wakati wanamgambo 37 wa Boko Haram wakiuawa katika operesheni hiyo, magaidi wengi walitoroka wakiwa na majeraha.

Akieleza kuwa makaazi ya magaidi yaliharibiwa kwenye operesheni hiyo, Gabkwet alitangaza kwamba risasi na silaha muhimu zinazomilikiwa magaidi pia zilikamatwa.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...