Katika mji wa Ebyan nchini Yemen, wanajeshi 2 walipoteza maisha na wengine 20 walijeruhiwa kwenye shambulizi la kombora lililotekelezwa katika msikiti wa kambi ya jeshi la serikali.
Kulingana na taarifa iliyopokewa kutoka kwa vyanzo vya ndani, kambi ya Brigade ya 5 ya jeshi la Yemen katika mji wa Ebyen ilishambuliwa kwa kombora.
Iliarifiwa kuwa wanajeshi 2 walipoteza maisha na wanajeshi 20 walijeruhiwa katika shambulizi lililolenga msikiti wa kambi hiyo wakati wanajeshi hao walikuwa wakisali sala ya adhuhuri.
Mohammed Kyizan, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari ya Yemen, alisema katika taarifa kwenye Twitter:
"Shambulizi la kigaidi la woga lilitekelezwa kwenye kambi ya 5 ya Brigade huko Ebyen wakati wanajeshi walikuwa wakifanya sala yao ya adhuhuri, na kulikuwa na watu waliouawa na waliojeruhiwa katika shambulizi hilo."
Wakati hakuna mtu aliyedai kuhusika na shambulizi hilo, hakuna habari iliyotolewa kutoka kwa mamlaka rasmi.

No comments:
Post a Comment