Viongozi na watu mbali mbali maarufu wamekuwa wakielekea katika makao makuu ya Kanisa la Nabii na muasisi wa kanisa la Synagogue Church of All Nations TB Joshua kwa siku ya pili kutoa heshima na rambi rambi zao kufuatia kifo chake.
Temitope Balogun Joshua aliyefahamika zaidi kama TB Joshua alifariki dunia mwezi uliopita akiwa na umri wa miaka 57.
Katika siku ya pili ya mchakato wa mazishi yake mke wake Evelyne na watoto wake watatu Sarah, Promise and Heart walipata fursa ya kumzungumzia maisha ya TB Joshua.
Kulingana na mke wake Evelyn Joshua, alishuhudiaTB Joshua akikua ‘’kutoka kuwa na kusanyiko la waumini 8 wa kanisa hadi kuwa na kanisa lililojaa umati wa watu na kuwa na wafuasi kote duniani "
‘’Alinifunza kuwa mwanamke niliye leo. Kwa dhahabu kuwa dhahabu lazima ipitie moto. Ninataka tu kukushukuru kwa kuwa baba mwema wa watoto wetu.", alisema mjane Everlyne.
Binti wa Marehemu TB Joshua Heart JoshuaImage caption: Binti wa Marehemu TB Joshua Heart Joshua
Watoto wake TB Joshua , Sarah, Promise na Heart walimsifu baba yao mpendwa kwa kuwa mtu aliyejitolea kumtumikia Mungu " kwa heshima bila uwoga."
"Aina ya upendo uliotuonesha hatukuwahi kuuona maishani mwetu. Kama kuna mtu yeyote aliyeishi maisha ya kushangaza ni wewe. Baba yangu alikuwa na utu ambao kwa namna ambayo sikuwahi kuelewa kamwe ," alisema binti yake Sarah.
Mchakato wa mazishi wa kumuenzi na kumkumbuka TB Joshua ulianza Jumatatu kwa kuwashwa kwa mishumaa.
Muhubiri huyo wa televisheni aliyekuwa maarufu Afrika, anatarajiwa kuzikwa Ijumaa wiki hii, katika mazishi ya faragha.

No comments:
Post a Comment