Search This Blog

Thursday, July 29, 2021

Wajumbe wa Taliban wakutana na waziri wa China


Timu ya wajumbe iliyoongozwa na Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Taliban nchini Qatar Mullah Abdul Ghani Birader, ilitembelea China.

Kulingana na habari ya Xinhua, Waziri wa Mambo ya Nje wa China Wang Yi alikutana na Mullah Abdul Ghani Birader katika jiji la Tianjin.

Wakati wa mkutano huo, Wang alisisitiza kuwa China, jirani yake mkubwa, imekuwa ikiheshimu uhuru, haki na uadilifu wa eneo la Afghanistan, na kusisitiza kwamba haipaswi kuingilia mambo ya ndani ya nchi hii.

Wang Yi alisema kuwa sera ya Afghanistan ya utawala wa Washington imeshindwa na kusisitiza kwamba pande zote nchini zinapaswa kuanzisha amani haraka iwezekanavyo kwa msingi wa kanuni kwamba "Afghanistan inapaswa kutawaliwa na Waafghanistan".

"Afghanistan ni ya watu wa Afghanistan, mustakabali na hatima ya Afghanistan inapaswa kuwa mikononi mwa watu wa Afghanistan," Wang alitumia maneno hayo.

Katika taarifa iliyotolewa na Taliban, ilielezwa kuwa timu ya wajumbe ya watu 9 walikwenda China kwa ziara ya siku mbili, na wakafanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa China juu ya mchakato wa amani na maswala ya usalama.

Mohammad Naim, msemaji wa Ofisi ya Kisiasa ya Taliban nchini Qatar, alisema kwenye mtandao wa Twitter, "Mazungumzo hayo yalilenga siasa, uchumi na usalama wa nchi zote mbili, na pia hali ya sasa nchini Afghanistan na mchakato wa amani."

Naim pia alibaini kuwa wajumbe wa Taliban waliihakikishia China kwamba hawatakubali eneo la Afghanistan litumike dhidi ya nchi yoyote ya kigeni.

Picha ya Wang na ujumbe wa Taliban pia ilichapishwa kwenye mitandao ya kijamii.

Wakati mchakato wa amani nchini Afghanistan bado haujabainika, mapigano makali kati ya vikosi vya usalama na Taliban yanaendelea.

 

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...