Search This Blog

Tuesday, July 13, 2021

TPLB yaitangaza simba kuwa mabingwa, kukabidhiwa kombe julai 18



Bodi ya Ligi Tanzania bara (TPLB) imetangaza kuwa klabu ya Simba ambao ndio mabingwa wa Ligi Kuu bara rasmi watakabidhiwa kombe la ubingwa msimu wa 2020-21, Julai 18 kwenye mchezo wa mwisho wa Ligi, jijini Dar es salaam.

Simba walitangazwa rasmi kuwa mabingwa wa VPL msimu wa 2020-21 na ubingwa wa nne mfululizo Jumamosi iliyopita Julai 11 baada ya kuifunga Coastal Unioni ya Tanga kwa mabao 2-0 na kufikisha alama 79 ambazo haziwezi kufikiwa na timu yoyote. Mabingwa hao wa Tanznaia wamebakiza michezo miwili ya Ligi dhidi ya Azam FC ndio mchezo unaofata utachezwa Julai 15 na watakabidhiwa kombe  kwenye mchezo wa Mwisho dhidi ya Namungo FC mchezo utakao chezwa uwanja wa Benjamini Mkapa.

Hii hapa taarifa rasmi iliyotolewa na bodi ya Ligi Tanzania bara kuhusu sherehe za kukabidhiwa ubingwa kwa klabu ya Simba SC.


 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...