Search This Blog

Wednesday, July 7, 2021

Rais Joe Biden ahimiza chanjo za covid-19 na kutoa tahadhari ya virusi aina ya Delta Marekani


Rais wa Marekani Joe Biden alisema kuwa virusi aina ya Delta ni hatari zaidi katika janga la corona (Kovid-19) na akahimiza kila mtu apewe chanjo.

Joe Biden alifanya tathmini juu ya vita dhidi ya janga la Kovid-19 na mpango wa chanjo katika Ikulu ya White House.

Akikumbusha kwamba walifikia kiwango cha dozi milioni 300 katika siku 150 za mchakato wa chanjo, Biden alibaini kuwa zaidi ya Wamarekani milioni 182 walipata angalau dozi ya 1 ya chanjo.

"Mwishoni mwa wiki hii, Wamarekani milioni 160 watapewa chanjo kamili. Hilo lilikuwa lengo nililoweka mnamo Machi na ninafurahi kuifanikisha ndani ya siku chache tu kuanzia Julai 4."

Akieleza kwamba kesi za maambukizi na vifo vya Kovid-19 vimepungua kwa asilimia 90, Biden alisema kuwa mamilioni ya Wamarekani ambao wamepewa chanjo kamili tangu Januari wamerudi katika hali yao ya maisha ya kawaida kama hapo awali, na kwamba biashara zimefunguliwa tena na ukuaji mkubwa wa uchumi unatabiriwa.

Biden pia alizungumzia vita dhidi ya janga hilo kama moja ya mafanikio makubwa katika historia ya Marekani na kusema,

"Mapambano yetu dhidi ya virusi hayajaisha. Hivi sasa, mamilioni ya Wamarekani bado hawajapewa chanjo na hawajapata kinga. Kwa hivyo, jamii zao ziko hatarini. Hii inaleta wasiwasi mkubwa zaidi kwa sababu ya virusi aina ya Delta."



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...