Search This Blog

Friday, July 23, 2021

Nigeria yapokea ndege sita za kupambana na waasi


Nigeria imepokea ndege sita za kijeshi iliyonunua kutoka Marekani, ambazo zinatarajiwa kupiga jeki juhudi za kukabiliana na makundi kadhaa yaliyojihami.

Ndege hizo aina ya A-29 Super Tucano zilitua katika mji wa kaskazini wa Kano siku ya Alhamisi na kupokelewa na Waziri wa Ulinzi Bashir Magashi na wakuu wengine wa kijeshi.

Nigeria ilikuw aimeagiza ndege kadhaa za kijeshi kutoka Marekani ambazo zilichukua miaka kadhaa kuundwa.

Ndege zingine sita zilizobakia zinatarajiwa kuwasili nchi mwezi Oktoba, Msemaji wa jeshi la anga la Nigeria Edward Gabkwet aliiambia BBC.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...