Namna sahihi ya kudumisha mahusianao yako ya kimapenzi na mwenza wako
aliye mbali nawe.
Siku zote mapenzi hupaswa kupewa thamani na nafasi kubwa kwa sababu yanaleta furaha katika maisha ya binadamu. Zipo sababu mbalimbali zinazopelekea mapenzi kuvunjika. Wapo baadhi ya wapenzi wanaoishi mahali tofauti na wenza wao.
Mambo mawili yanaweza kuwa mbalimbali kama masomo na kazi.
Umbali baina ya wapenzi hufanya penzi kutetereka kama wapendanao hawatofanya kazi ya ziada kuhakikisha wanaziba mianya yote itakayosababisha usaliti.
Mapenzi ya mbali ni vigumu kutetereka endapo tu wapenzi watakuwa wanapendana kwa dhati na kutamani kuwa pamoja wakati wote na mmoja wapo kuamua kujitoa muhanga na kuhamia anakoishi au kufanyia kazi mwenzake.
Hata hivyo mnaweza kudumisha mapenzi kama mtaamua kuyafuata haya:-
Mawasiliano ya mara kwa mara
Hii ni njia muhimu sana baina ya wapendanao humfanya mtu ahisi uwepo wa mpenzi wake hata kama atakuwa mbali naye. Hivyo kama unae mpenzi wako aliye mbali hakikisha unawasiliana naye mara kwa mara kwa kutumi email,sms ,kadi au simu.
Heshimu hisia zako
Mapenzi ya kweli yametawaliwa na hisia kali za mapenzi ,kama huna hisia za kweli unajikuta hufurahii mapenzi hutapata raha ipasavyo.Hivyo hakikisha unamtunzia penzi lake mpaka pale mtakapokutana hata kama uko masomoni ama kazini.
Uaminifu pekee ndiyo utakaofanya uwasiliane nae mara kwa mara.

No comments:
Post a Comment