Mapambano makali ya miezi minane ya kuwania udhibiti wa mji wa kaskazini wa Tigray nchini Ethiopia yameenea mpaka kwenye mji jirani wa Afar katika kipindi cha juma lililopita.
Takribani raia 20 wameuawa na watu 54,000 wamekimbia makazi yao, ripoti zinasema, huku hofu ikiongezeka kuhusu kuongezeka kwa kasi kwa mzozo wa kibinadamu.
Watu kahaa mjini Afar wameiambia BBC kuwa wassi wa TPLF wamewaua raia.
Madai haya hayajathibitishwa
BBC pia imesikia ripoti za kuwepo kwa mashambulizi ya anga yaliyolenga maeneo ya waasi wa TPLF mjini Afar siku chache zilizopita.
TPLF wanapambana na jeshi la Ethiopia na washirika wake mjini Afar, mji ulio kwenye mpaka na Tigray . Msemaji wa Afar amesema wapiganaji wa Tigray waliteka wilaya tatu mjini humo wiki hii.
Wanaharakati wa mjini Afar wamesema kunahitajika chakula,maji na malazi ya dharura.

No comments:
Post a Comment