Mapigano makali yanaripotiwa kuendeleakatika jimbo la Afar nchini Ethiopia ambako maelfu ya watu wamesambaratishwa
Huku mzozo wa muda mrefu ukiendelea katika jimbo la Tigray, mzozo huo una unaendelea kusambaa katika majimbo mengine ya nchi.
Katika jimbo la Tigray, ripoti zinasema kumekuwa na mapigano makali kwa siku siku nne mfulurizo zilizopita .
Waasi waTigray People’s Liberation Front (TPLF) wanakabiliana na vikozi vya jimbo la na washirika wake.
Wakazi wa jimbo la Afar waliozungumza na BBC wamedai kuna majeruhi wengi katika eneo hilo kutokana na mashambulio ya wapiganaji waasi wa TPLF.
Hatahivyo, msemaji wa TPLF alitoa taarifa kupitia mtandao wa Twitter akisema chama hicho hakiko vitani na watu wa Afar au wapiganaji, bali viongozi wa Ethiopia.
Wanaharakati katiak jimbo la Afar wanasema msaada wa dharura w akibinadamu unahitajika kwa wakulima wa eneo hilo na watu wengine walio lazimishwa kukimbia kufuatia mapigano.

No comments:
Post a Comment