Search This Blog

Thursday, July 29, 2021

Mapigano yapamba moto Amhara wakati vita vya Ethiopia vikiendelea


Mapigano makali yameripotiwa mkoani Amhara nchini Ethiopia- ishara kuwa vita vya Tigray vinasambaa katika mikoa ya jirani.

Maafisa mjini Amhara wamesema majeshi ya serikali na vikosi vya Amhara vimehusika katika mapigano dhidi ya waasi wa Tigray People’s Liberation Front (TPLF).

Hatua hii inakuja wakati mji ikiendelea kutuma vikosi vyake kupambana na TPLF.

Pamoja na hayo, msemaji wa Waziri Mkuu Abiy Ahmed alisema makubaliano ya usitishaji mapigano uliotangazwa mwezi uliopita hayakutekelezwa.

Serikali na waasi wa TPLF wamenyoosheana vidole kwa kuchangia kuongezeka mzozo.

Katika hali tofauti, mamlaka katika mkoa wa magharibi wa Benishangul-Gumuz zinasema vikosi vya usalama vimewaua zaidi ya wapiganaji 100 wenye silaha ambalo limekuwa likitekeleza mashambulizi mengi ya kikabila.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...