Watu wasiopungua 800 katika nchi ya Afrika Mashariki ya Uganda wameripotiwa kupewa chanjo bandia za corona.
Ilitangazwa kuwa chanjo bandia zilitumiwa zaidi katika hospitali za kibinafsi karibu na mji mkuu wa Kampala kati ya Mei 15 na 18 Juni.
Warren Namara, afisa wa afya ambaye alitoa taarifa juu ya suala hili alisema:
"Kufikia katikati ya mwezi Mei, idadi ya watu waliopokea chanjo bandia ni angalau 800. Bidhaa hii inaweza kuwa imepewa watu wengi zaidi."
Iliripotiwa kuwa watu 2 walikamatwa na kuzuiliwa kuhusiana na tukio hilo, na daktari aliyehusika anatafutwa.
Kulingana na data ya Wizara ya Afya ya Uganda, zaidi ya kesi 79,000 za Covid-19 zimegundulika nchini humo hadi kufikia sasa, na karibu watu 900 walipoteza maisha kutokana na virusi. Idadi ya dozi za chanjo zilizotolewa imezidi 843,000.

No comments:
Post a Comment