Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Mohamed Hassan Moyo amesema Makandarasi watakaojenga chini ya kiwango Miradi ya Kimaendeleo katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa watarudia kwa gharama zao kwa ubora ule ule unatakiwa kutokana na thamani ya mradi husika
Moyo amesema miradi mingi imejengwa kwa viwango vinavyotakiwa ila tatizo kubwa lipo kwa Makandarasi ambao wamekuwa wakipewa Tenda za Ujenzi wa Miradi wanaichelewesha kwa makusudi na kusababisha kuchelewa kuanza kufanya kazi kwa miradi hiyo
Aliwataka watendaji wote wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa kuhakikisha wanafanya kazi kwa weledi ili kutumia Fedha za Wananchi vizuri kuendana na mradi ambao unakuwa unatekelezwa kwenye maeneo yao
No comments:
Post a Comment