Search This Blog

Wednesday, July 28, 2021

Jeshi lafutilia mbali matokeo ya uchaguzi Myanmar


Jeshi, ambalo lilinyakua serikali iliyochaguliwa katika mapinduzi ya kijeshi huko Myanmar, liliamua kuwa matokeo ya uchaguzi mkuu wa tarehe 8 Novemba 2020 yalikuwa batili.

Thein Soe, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Muungano (UEC) iliyoanzishwa na utawala wa jeshi baada ya mapinduzi ya Februari 1, alitangaza kwamba wamekamilisha uchunguzi wa madai kwamba chama cha National Democratic Union (NLD) cha Suu Kyi,, kilihusika na udanganyifu katika uchaguzi wa 2020 .

MWenyekiti wa UEC Soe alisema kuwa waligundua udanganyifu katika zaidi ya kura milioni 11.

Akieleza kuwa madai juu ya ushindani usiofaa katika uchaguzi na udanganyifu katika hesabu za kura baada ya uchaguzi yamekuwa ya mwisho, Soe alisema,

"Matokeo ya uchaguzi wa 2020, ambao haukufanyika katika mazingira huru na ya haki, yamefutwa."

Soe hakutoa taarifa juu ya tarehe mpya ambayo uchaguzi mkuu utafanyika.

Katika uchaguzi mkuu uliofanyika Myanmar mnamo Novemba 8, 2020, chama cha NLD cha kiongozi wa zamani wa nchi hiyo na Waziri wa Mambo ya Nje Suu Kyi, kilihifadhi nguvu zake kwa kushinda viti 238 katika Bunge na viti 138 katika Seneti.

Jeshi la Myanmar lilichukua madaraka mnamo Februari 1, baada ya madai ya udanganyifu katika uchaguzi mkuu wa 2020 na mvutano wa kisiasa nchini humo.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...