Search This Blog

Thursday, July 8, 2021

Idadi ya kesi za maambukizi ya covid-19 kwa siku yaongezeka nchini Korea Kusini


Kesi 1212 za maambukizi ya Kovid-19 zilizogunduliwa Korea Kusini ndani ya masaa 24 yaliyopita zilirekodiwa kama idadi kubwa ya kesi za kila siku tangu 25 Desemba 2020.

Kulingana na taarifa iliyotolewa na Kituo cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa cha Korea Kusini, kesi 1212 za maambukizi ya Kovid-19 ziligunduliwa ndani ya masaa 24 yaliyopita na kufikia kiwango kikubwa zaidi kwa kesi za kila siku tangu Desemba 25, 2020.

Nchi hiyo ambapo idadi ya kesi ziliongezeka kwa 1212 na kufikia 162,753, idadi ya vifo kutokana na virusi pia iliongezeka hadi 2,033, na mtu mmoja alipoteza maisha ndani ya masaa 24 yaliyopita. Idadi ya watu waliopona nchini humo ilirekodiwa kuwa 151,500.

Wakati idadi ya kesi zinazopanda nchini zinaonekana kama ishara ya wimbi la nne, Waziri Mkuu Kim Boo-kyum alitangaza kwamba sheria ya kuzingatia masafa ya umbali wa kijamii iliyoletwa ndani ya wigo wa hatua za Kovid-19 imeongezwa kwa angalau wiki moja zaidi katika mji mkuu wa Seoul.

Kim alisema kuwa janga hilo kwa ujumla linaonekana katika kundi la umri wa miaka 20-30 ambao hawajapewa chanjo.

Mikusanyiko ya zaidi ya watu 5 pia hairuhusiwi chini ya hatua za sasa nchini humo.

Katika nchi ya Korea Kusini, mnamo Desemba 25 wakati wimbi la tatu lilionekana, idadi kubwa zaidi ya kesi za maambukizi ilionekana tangu mwanzo mwa janga hilo na kurekodiwa kama 1240.

Kwa upande mwingine, ilielezwa kuwa wakati dozi za kwanza za chanjo ya Kovid-19 zilipewa kwa takriban watu milioni 15.4 nchini, watu milioni 5.4 pia walipokea dozi za pili za chanjo.

Katika nchi ya China, mamlaka ilitangaza kwamba amri ya kutotoka nje ilitangazwa katika jiji la Ruili, ambalo liko kwenye mpaka wa Myanmar, baada ya kuongezeka kwa kesi za maambukizi ya Kovid-19.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...