Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) Tedros Adhanom Ghebreyesus, alisema kwamba amepokea vyema tangazo la nchi za G7 la kutoa dozi milioni 870 za chanjo ya corona(Covid-19) kwa nchi zinazohitaji, ingawai hatua hiyo haitoshelezi.
Katika taarifa iliyoandikwa na kutolewa na WHO, iliarifiwa kwamba G7 itatoa dozi milioni 870 za chanjo moja kwa moja kwa Mpango wa Ufikiaji wa Chanjo za Covid-19 Ulimwenguni (COVAX), na kwamba angalau nusu ya msaada huu utatolewa hadi mwisho wa mwaka huu na sehemu iliyobaki hadi mwaka 2022.
Ikisisitiza kuwa nchi za G7 zilithibitisha tena msaada wao kwa COVAX, ilibainika kwamba COVAX ndio mpango wa kipaumbele katika usambazaji wa chanjo kwa nchi masikini zaidi.
Ghebreyesus, ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa WHO, alitoa maoni yake juu ya uamuzi wa G7 kwa kusema,
"Nchi nyingi kwa sasa zinakabiliwa na ongezeko la kesi za maambukizi na kukosa chanjo. Sote tuko kwenye mbio za maisha yetu, lakini sio haki. Nchi nyingi bado hazijaanza mchakato."
Ghebreyesus alikaribisha uamuzi wa ukarimu wa G7 kutoa chanjo, akiongezea kusema, "Lakini tunahitaji zaidi na tunahitaji kupata chanjo hizi haraka."

No comments:
Post a Comment