Watu wasiopungua 11 walifariki kwenye mlipuko uliotokea kwenye bomba la gesi asilia katika mkoa wa Hubei nchini China.
Mamlaka ilitangaza kuwa mlipuko huo ulitokea kwenye bomba la gesi asilia mwendo wa saa 06:30 kwa saa za ndani katika eneo la makaazi lililoko mji wa Shiyen huko Hubei.
Iliripotiwa kuwa watu wasiopungua 11 walipoteza maisha na wengine 37 walijeruhiwa katika mlipuko huo.
Timu za Afya zilitoa maelezo kwamba watu 144 walioathiriwa na mlipuko huo ikiwa ni pamoja na 37 waliojeruhiwa, wamelazwa hospitalini.
Wakati timu za utaftaji na uokoaji zinaendeleza shughuli zao katika eneo la tukio, kuna wasiwasi kwamba idadi ya vifo huenda ikaongezeka.
Hakuna taarifa rasmi iliyotolewa kuhusu chanzo cha mlipuko huo.

No comments:
Post a Comment