Takriban watu 15 wameuawa katikati mwa Burundi, ripoti za vyombo vya habari nchini humo zinaripoti.
Shambulio hilo Jumamosi jioni lilikuwa katika mkoa wa Muramvya, ambapo watu 12 walifariki katika shambulio kama hilo mwezi Mei.
Kulingana na walioshuhudia tukio hilo, watu wenye silaha walifunga barabara kwa mawe makubwa wakati wa giza kisha wakayafyatulia risasi magari hayo.
Mabasi mawili yalichomwa moto. Abiria kadhaa waliojeruhiwa walipelekwa hospitalini.
Wizara ya mambo ya ndani ya Burundi ilielezea shambulio hilo kuwa la ugaidi. Haijulikani ni nani aliyehusika

No comments:
Post a Comment