Search This Blog

Monday, June 28, 2021

Watu waliojihami waua watu 15 na kuchoma moto mabasi Burundi


Takriban watu 15 wameuawa katikati mwa Burundi, ripoti za vyombo vya habari nchini humo zinaripoti.

Shambulio hilo Jumamosi jioni lilikuwa katika mkoa wa Muramvya, ambapo watu 12 walifariki katika shambulio kama hilo mwezi Mei.

Kulingana na walioshuhudia tukio hilo, watu wenye silaha walifunga barabara kwa mawe makubwa wakati wa giza kisha wakayafyatulia risasi magari hayo.

Mabasi mawili yalichomwa moto. Abiria kadhaa waliojeruhiwa walipelekwa hospitalini.

Wizara ya mambo ya ndani ya Burundi ilielezea shambulio hilo kuwa la ugaidi. Haijulikani ni nani aliyehusika



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...