Search This Blog

Tuesday, June 15, 2021

Simba ipo kamili kuivaa Polisi Tanzaania


 UONGOZI wa Simba umeweka wazi kwamba upo tayari kwa ajili ya mechi zao ambazo zimebaki ndani ya ligi ikiwa ni pamoja na ule dhidi ya Polisi Tanzania.

Mchezo wao ujao kwenye ligi unatarajiwa kuchezwa Uwanja wa Ushirika, Moshi baada ya ule wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Mkapa ubao kusoma Simba 2-0 Polisi Tanzania.

Akizungumza na Spoti Xtra, Meneja wa Simba, Patrik Rweyemamu alisema kuwa maandalizi ya kikosi kwa mechi ambazo zimebaki yapo vizuri.

“Tupo vizuri kwa ajili ya mechi zetu ambazo zimebaki na mchezo wetu ujao pia tunaamini kwamba tutapambana ili kupata pointi tatu, mashabiki watupe sapoti kwani timu ilianza mazoezi Juni 8,” alisema Rweyemamu.

Kwenye msimamo wa ligi, Simba ipo nafasi ya kwanza ikiwa na pointi 67 inakwenda kukutana na Polisi Tanzania iliyo nafasi ya 6 na pointi 41



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...