Search This Blog

Monday, June 14, 2021

Rais wa Zambia 'hana neno' baada ya kuzimia


Rais wa Zambia Edgar Lungu amewahakikishia wananchi kwamba hana neno baada ya kuzimia akihudhuria mkutano wa hadhara.

Alikuwa akiongoza siku ya ulinzi hapo jana (Jumapili) mara "ghafla akashikwa na kisunzi"mjini, Lusaka.

Katibu wa baraza la mawaziri Simon Miti alitoa taarifa akisema rais ''ni mzima na anaendelea na shughuli zake za kazi".

Dkt Miti anasema Rais Lungu alipata nafuu mara moja baada ya tukio hilo.

Rais alikabiliwa na hali kama hiyo ya kiafya mwaka 2015 na wakati huo ofisi yake ilisema kwamba ilitokana tatizo katika umio wake.

Rais Lungu anagombea tena uongozi wa nchi hiyo katika uchaguzi mkuu utakaoandaliwa tarehe 12 mwezi Agosti.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...