Rais wa Pakistan Arif Alvi ameishutumu serikali ya India kwa kujaribu kuvuruga uhusiano kati ya Islamabad na Kabul.
Alvi alizungumza na vyombo vya habari vya India na kusema kwamba India inataka kutengeza hali ya ukosefu wa maelewano na Pakistan nchini Afghanistan.
Akibainisha kuwa India ina jukumu la kusababisha usumbufu, Alvi alisema kwamba New Delhi kwa muda mrefu imekuwa ikitaka kuvuruga uhusiano kati ya Islamabad na Kabul.
Alvi pia alitoa jibu kwa Mshauri wa Usalama wa Rais wa Afghanistan Ashraf Ghani, Hamdullah Muhib, kwa taarifa zake dhidi ya Pakistan na kukumbusha kuwa nchi yake inahifadhi wakimbizi milioni 3,5 wa Afghanistan.
Akisisitiza kwamba maafisa wa serikali ya Afghanistan wanapaswa kutoa matamshi kwa umakini, Alvi pia alisema kuwa hawapaswi kulaumu Pakistan kwa makosa yao wenyewe.
Muhib, Mshauri wa Usalama kwa Rais wa Afghanistan Ashraf Ghani, na maafisa wengine wa Afghanistan walitoa taarifa kwamba Pakistan ilihusika na wimbi la mashambulizi yaliyofanywa na Taliban dhidi ya vikosi vya usalama.
Pakistan, kwa upande mwingine, ilijibu maoni haya na maafisa wa Afghanistan na wakakanusha madai hayo.

No comments:
Post a Comment