Search This Blog

Friday, June 25, 2021

Padri akamatwa kwa shutuma za wizi wa mamilioni ya pesa


Ofisi ya upelelezi ya Rwanda (RIB) imethibitisha kuwa inamshikilia Mkuu wa makasisi wa Kanisa katoliki Parokia ya Rwamagana nchini humo, Jean-Marie Telesphore Ingabire, ambaye anashukiwa kusaidia katika madai ya wizi na kufich ushahidi.

Msemaji wa RIB, Thierry Murangira, ameiambia BBC, kuwa Padre Ingabiri amekamatwa na mamilioni ya fedha yanayodaiwa kuwa ni ya wizi.

"Mkuu wa mapadri wa Parokia ya Rwamagana ya Kanisa Katoliki yuko mahabusu, anashutumiwa wa kusaidia katika madai mashitaka ya wizi, huku uchunguzi ukiendelea,” amesema Murangira.

Vyombo vya habari nchini Rwanda vilituma taarifa ya kukamatwa kwa Padri Jean-Marie Telesphore Ingabire kupitia Twitter:

Uchunguzi bado unaendelea kubaini kiasi cha pesa kilichohusika, alisema Bw Murangira na kuongeza kuwa kasisi huyo alikuwa akitunza pesa haramu zinazodaiwa kuibwa, jambo lililowafanyawaendelee na wizi.

Vyanzo mbalimbali vinaonesha kuwa watu kadhaa walikamatwa tangu mwishoni mwa wiki iliyopita kwa tuhuma za wizi , akiwemo ndugu zake Padre Ingabire ambao walipatikana wakiwa wamejifichana "kiwango kikubwa cha fedha ."

Kasisi huyo anasemekana kushindwa kuelezea ni kwa vipi alikuwa na mamilioni ya fedha nyumbani kwake, wakati msako ulipofanyika kwenye makazi yake.

Murangira amsema kuwa RIB inatarajia kupata maelezo zaidi wakati uchunguzi ukiendelea.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...