Search This Blog

Thursday, June 24, 2021

Mashambulizi mapya ya wanamgambo yaripotiwa Msumbiji


Wanamgambo wa kijihadi wamehusika tena katika mashambulio mapya karibu mji wa Palma kaskazini mwa Msumbiji, vyanzo vya habari vya jeshi vimeliambia shirika la habari la AFP.

Shambulio hilo linakuja wakati ambapo nchi za kusini mwa Afrika zimeishinisha kupelekwa kwa kikosi maalum kusaidia Msumbijikukabiliana na wanamgambo hao.

"Wanamgambo hao walijaribu kushambulia ngome za vikosi vya serikali mjini in Patacua, karibu na eneo la Afungi LNG lakini walirudishwa nyuma baada ya kupatikana kwa msaada kutoka angani," shirika la habari la AFP lilinukuu vyanzo vya habari vikisema.

Mkoa wa kaskazini Cabo Delgado kwa muda mrefu umekuwa ukikabiliwa na changamoto kadhaa lakini uvamizi kutoka kwa wanamgambo wa kijihadi ulianza mwaka 2017.

Mzozo huo umevuti ajamii ya kimataifa baada ya wanamgambo kuteka mji wa Palma mwezi April, kuua raia wa kigeni na kukwamisha mradi wa gesi asilia wa thamani ya dola bilioni 20 za Kimarekani.

Mashambuilo ya wanamgambo yamesababisha mzozo mkubwa wakibinadamu, huku watu waliofurushwa makwaowakiishi katika kambi za wakimbizi karibu na mikoa inayozunguka Cabo Delgado.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...