Search This Blog

Wednesday, June 30, 2021

Jifunze namna ya kumuacha mpenzi wako kistrabu

 


Inapofika mahali umemchoka mpenzi wako ni bora umwambie kwa maneno matupu tena ya bila kupindisha kwamba nimekuchoka sikutaki tena sitaki mahusiano na wewe tena nenda zako, ukieleza kifupi hivyo utaeleweka vizuri tu na kama huyo unaemwambia ana akili timamu wala hawezi kuendelea tena na mahusiano na wewe au kukulilia kama vile wewe ni mungu kwake ikiwa umemtamkia maneno mazito kama hayo.

Lakini tabia ya kuachana kwa maneno mazito yenye matusi mazito mazito yanayohusisha mpaka na wazazi na ndugu wengine ambao hawayajui hata mahusiano yenu tabia hii huwa sio nzuri kabisa, kwanza inaonyesha hujakua hata kidogo na akili yako finyu na ndogo kama tonge la ugali wa mtama.

Mwanamke au mwanaume aliekuwa ki akili cha kwanza ni lazima kinywa chake kiumbwe na maneno ya busara, hekima na adabu, no matter how/haijalishi mmeudhiana vipi katika mahusiano na mmefikia stage ya kuachana ni lazima muachane kwa busara, tabia ya kukamuliana matusi kama chunisi dume au ndimu kwenye samaki kukata shombo inaprove kwamba wewe ni zero brain kiasi gani katika maisha yako.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...