Search This Blog

Sunday, June 27, 2021

DC Kisarawe aanza na wajawazito

Mkuu wa wilaya ya Kisarawe Mhe. Nickson Simon ameendesha zoezi la uchangishaji damu katika hospitali ya wilaya ya Kisarawe, ikiwa ni sehemu ya kutatua changamoto kubwa ya vifo vinavyotokana na upungufu wa damu inayowakabili akina mama wajawazito na watoto wakati wa kujifungua.

Akizunguma katika zoezi la uchangishaji damu lililoshirikisha wamiliki wa magari ya Forester's National Tanzania na Subaru mkuu wa wilaya Mh. Nickson Simon amewashukuru wachangiaji hao.

Amesema msaada huo unakwenda kuwachachu ya kuwaibua wachangiaji wengine kujitokeza ili kuondokana na tatizo la upungufu wa damu linaloikabili hospitali hiyo.

Kwa upande mwingine baadhi ya washiriki katika zoezi hilo wameahidi kuendelea kujitolea damu kwa wenye uhitaji.


 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...