Search This Blog

Wednesday, June 23, 2021

Askari amuua mwenzake kwa risasi wakiwa lindoni Moshi “amekimbia”


Jeshi la polisi mkoani Kilimanjaro kupitia kwa kamanda wa polisi Amoni Kakwale, limethibitisha kufariki kwa askari wa Suma JKT Emmanuel Malya anayedaiwa kuuawa na askari mwenzake aliyekuwa naye kwenye lindo la TANESCO eneo la Moshi.

Kakwale amesema waliukuta mwili wa marehemu ukiwa na majeraha ambapo wanaendelea kumtafuta askari mwenzake aliyekimbia ambapo walikuwa wote.

“Tulifika eneo la tukio nakukuta mwili wake ukiwa na majeraha na silaha yake aina ya shortgun pump action ikiwa pembeni, baada ya uchunguzi tulibaini alikuwa na mwenzake na alikimbia na tunaendelea kumtafuta”-Kakwale RPC Kilimanjaro



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...