Kiongozi wa kundi la wanamgambo wa Boko Haram nchini Nigeria Abubakar Shekau, amejiua mwenyewe , wanamgambo wa kundi hasimu wamesema katika sauti iliyorekodiwa.
Katika rekodi ya sauti iliyopatikana na mashirika ya habari, kundi la Islamic State katika mkoa wa Afrika Magharibi (Iswap) lilisema Shekau alifariki baada ya kujilipua kwa kutumia vilipuzi wakati wa mapigano kati ya makundi hayo mawili.
Katika sauti ambayo haikuwa na tarehe iliyorekodiwa, sauti inayodhaniwa kuwa ya kiongozi wa Iswap Abu Musab al-Barnawi ilisema Shekau "alijiua kwa kujilipua na vilipuzi".
Wapiganaji wa Iswap walimsaka mbabe huyo wa kivita na kumpatia nafasi ya kutubu na kujiunga nao, al-Barnawi alisema.
"Shekau alipendelea kudhalilishwa katika maisha ya baadaye kuliko kudhalilika duniani," alisema.
Wakati ripoti za kifo cha Shekau katika mapigano ziliposambazwa mwezi uliopita, jeshi la Nigeria lilisema litachunguza.
Msemaji wa jeshi Brigedia Jenerali Mohammed Yerima aliiambia BBC wakati huo kwamba jeshi lilikuwa linachunguza kile kilichotokea, lakini halitatoa taarifa hadi lipate uthibitisho rasmi.
Mwandishi mmoja aliye na uhusiano wa karibu na vyombo vya usalama alisema kuwa Shekau alikufa wakati Iswap iliposhambulia ngome za Boko Haram katika msitu wa Sambisa, kaskazini mashariki mwa Nigeria
Baada ya kuchukua uongozi wa of Boko Haram mwanzilishi wake alipofariki katika kizuizi cha polisi mwaka 2009, Shekau aliongoza mabadiliko yake kutoka kwa dhehebu la kawaida hadi uasi mbaya ambao umeenea kaskazini-mashariki mwa Nigeria.

No comments:
Post a Comment