Search This Blog

Sunday, May 16, 2021

WHO yatangaza kuwa janga la Covid-19 litakuwa hatari zaidi mwaka huu kuliko mwaka jana

 


Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) limesema kwamba mwaka wa 2021 utakuwa "mbaya zaidi" kwa sababu ya janga la corona (Covid-19), lililoibuka China mwishoni mwa mwaka 2019 na likageuka kuwa janga kubwa kwa kuenea kote ulimwenguni mnamo 2020.

Mkurugenzi Mkuu wa WHO Tedros Adhanom Ghebreyesus alisema,

"Tunaamini mwaka wa pili wa janga hili utakuwa mbaya zaidi kuliko ule wa kwanza."

Akibainisha kwamba wimbi la pili la janga hilo nchini India "limeleta wasiwasi mkubwa", Ghebreyesus alisema kuwa "visa vipya vya kutisha, kulazwa hospitalini na vifo" vilirekodiwa katika majimbo mengi ya India.

Ghebreyesus alisema kuwa kama WHO, walituma bomba la oksijeni India, mahema, barakoa na vifaa vya matibabu kwa hospitali za mikoani.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...