Search This Blog

Monday, May 31, 2021

Wanafunzi 14 waliotekwa nyara kutoka chuo kikuu cha kibinasi nchini Nigeria waachiliwa


Wanafunzi 14 waliotekwa nyara na watu wenye silaha kutoka chuo kikuu cha kibinafsi mnamo Aprili 20 katika jimbo la Kaduna nchini Nigeria, wameachiliwa.

Kamishna wa Usalama wa Ndani na Mambo ya Ndani wa Jimbo la Kaduna Samuel Aruwan alitangaza kuachiliwa kwa wanafunzi 14 waliotekwa nyara kutoka Chuo Kikuu cha kibinafsi cha Green Field.

Aruwan ambaye hakutoa taarifa zaidi juu ya namna wanafunzi hao walivyoachiliwa, alieleza kuwa wasilishwa kwa familia zao.

Watu wenye silaha waliwateka nyara wanafunzi 19 katika shambulizi la Chuo Kikuu cha kibinafsi cha Green Field mnamo Aprili 20. Wanafunzi watano kati ya yao walipatikana wakiwa wamekufa karibu na chuo mnamo Aprili 23.

Gavana wa jimbo la Kaduna, Nasir Ahmad al-Rufai, alitangaza kwamba hatalipa fidia iliyodaiwa kwa ajili ya kuachiliwa kwa wanafunzi.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...