Spika wa Bunge Job Ndugai, leo Jumatatu Mei 24, 2021 amewaapisha wabunge wawili waliochaguliwa hivi karibuni katika majimbo ya Mkoa wa Kigoma.
Wabunge hao ni Dk Florence Samizi wa jimbo la Muhambwe na Kavejuru Felix wa la Buhigwe, wote wakitokea CCM.
Mbunge wa Buhigwe, Kavejuru Eliadory Felix akila kiapo cha uaminifu na utii bungeni mbele ya Spika wa Bunge, Job Ndugai, jijini Dodoma leo. Picha na Edwin Mjwahuzi
Wabunge hao wameapishwa baada ya ushindi waliopata katika uchaguzi mdogo uliofanyika kwa majimbo hayo kuwa wazi kufuatia kifo cha aliyekuwa mbunge wa Muhambwe, Atashasta Nditiye na Dk Philip Mpango wa Buhigwe aliyeteuliwa kuwa Makamu wa Rais.
Licha ya kusindikizwa na wabunge wengi, hakukuwa na shamrashamra kubwa kama ambavyo imezoeleka katika uapisho wa wabunge wanaochaguliwa kwenye chaguzi ndogo

No comments:
Post a Comment