Rais wa zamani wa Marekani (USA) Donald Trump, ambaye akaunti zake zilisimamishwa hapo awali kwenye majukwaa ya mitandao ya kijamii, ameanzisha blogi ya kibinafsi.
Trump aliitambulisha blogi yake ya jina la "Meza ya Donald Trump" kama "mahali pa kuzungumza kwa uhuru na usalama".
Kwa njia hii, Donald Trump ataweza kuwasiliana moja kwa moja na wafuasi wake.
Kwenye wavuti, watumiaji wana fursa ya kuonyesha kupenda machapisho ambayo Trump aliwahi kuyachapisha kwenye Twitter na Facebook.
Hii inachukuliwa kama mpango wa Rais wa zamani wa kutaka kufikia Facebook na Twitter.
Bado haijafahamika ikiwa mashirika husika yataruhusu machapisho ya Donald Trump kuhamishiwa kwenye majukwaa mengine ya mitandao ya kijamii.
Baada ya uvamizi wa Bunge na umwagaji damu uliotokea mnamo Januari 6, majukwaa makubwa ya teknolojia yalisimamisha akaunti za mitandao ya kijamii za Donald Trump na kuzuia machapisho yake.
Trump alitangaza kuwa ataanzisha mtandao wake wa kijamii.

No comments:
Post a Comment