Search This Blog

Monday, May 10, 2021

Shambulizi la kujitoa muhanga Somalia,Watu sita wamepoteza maisha

Watu sita, wakiwemo polisi 2, wamefariki katika shambulizi la kujitoa muhanga ambapo kituo cha polisi kililengwa huko Mogadishu, mji mkuu wa Somalia.

Vyombo vya habari vya serikali ya Somalia vimeripoti kuwa shambulizi la kujitoa muhanga lilitekelezwa katika kituo cha polisi katika wilaya ya Waberi ya Mogadishu.

Taarifa iliyoandikwa na polisi imesema, "Watu sita, pamoja na Mkuu wa Polisi Ahmed Bashane na Naibu Kamanda Idara Abdi Basid, wamepoteza maisha katika shambulizi la kujitoa muhanga lililolenga kituo cha polisi katika mkoa wa Waberi."

Hakuna mtu aliyedai kuhusika na shambulizi hilo, lililolaaniwa na Waziri Mkuu Hüseyin Roble kupitia Twitter.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...