Serikali imesema kuwa sasa ni wakati sahihi wa kuanza kupeleka fedha za michezo ngazi za chini ambazo zitatumika kuongeza kasi ya maendeleo ya michezo mbalimbali nchini.
Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bi Pauline Gegul wakati wa ufunguzi wa Kongomano la Wadau wa Michezo Mkoani Manyara lililoratibiwa na Wilaya ya Babati.
“Kwa sasa fedha ya maendeleo ya michezo inayopelekwa katika ngazi ya chini na shuleni ni ile ya uendeshaji wa shule kwa shule zetu za msingi na sekondari tu na inaitumika kwa ajili ya manunuzi ya vifaaa vya michezo” amesema Mheshimiwa Gekul.
Ameongeza kuwa Waziri mwenye dhamana ya Habari, Utamaduni ,Sanaa na Michezo Mheshimiwa Innocent Bashungwa amekutana na Waziri wa Mipango na Fedha Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Nchemba kwa lengo la kuanzisha Mfuko wa Maendeleo ya Michezo ambao kwa sasa bado suala hilo linafanyiwa kazi kwa kina juu ya vyanzo vyake vya fedha.
“Jukumu lenu nyinyi kama wadau wa michezo mara tu mfuko huu ukianzishwa basi kila mmoja wetu achangie ili kuweza kufanikisha lengo hilo la kukuza michezo kwa taifa letu”alihimiza Mheshimiwa Gekul.
No comments:
Post a Comment