Imekuwa ni kama desturi sasa kwa ma-staa kutokea nchini marekani kuripotiwa kumwaga mamilioni ya dola kwa ajili ya kununua vito vya thamani kama vile vyeni, vipuli, saa N.k
Star hip-hop kutokea nchini Marekani Rick Ross amechapishwa kwenye moja ya taarifa na tovuti ya habari za burudani nchini humo #DailyLoud akiripotiwa kununua cheni ya Almasi yenye thamani ya dola za Marekani $500,000 ambazo ni takribani Bilioni 1.15 kwa fedha za Tanzania 🇹🇿
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na tovuti hiyo, cheni hiyo ilionekana na chapa ya label yake ya muziki "Maybach Music Group" @untouchablemmg iliyotengenezwa na sonara maarufu #JonnyDanny
Hii si mara kwanza kwa RickRoss kununua vito vya kwa Sonara huyu, pia aliwahi kumwaga mabilioni ya fedha kwa ajili ya saa iliyomgharimu kiasi cha Bilioni 41 za kitanzania

No comments:
Post a Comment