Search This Blog

Thursday, May 27, 2021

Rais Macron azuru Rwanda kurekebisha uhusiano wa kidiplomasia

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron anazuru Rwanda katika jaribio la kufufua uhusiano ambao ulisambaratika kufuatia tuhuma juu ya jukumu la Paris katika mauaji ya kimbari ya 1994.

Ziara hiyo inafuatia hatua ya Ufaransa kutoa ripoti rasmi mwezi Machi inayokiri kuwa serikali ya wakati huo ya Francois Mitterrand "ilizembea" kwa kutotabiri mauaji hayo.

Ripoti hiyo, ambayo imekaribishwa Kigali, imeiondolea Ufaransa jukumu la moja kwa moja katika mauaji ya zaidi ya Watutsi 800,000 na Wahutu wenye msimamo wa wastani.

Rais wa Rwanda Paul Kagame, Hivi karibuni alisema Wanyarwanda hawatasahau lakini wanaweza kuisamehe Ufaransa kwa jukumu lake na kuashiria kwamba Paris na Kigali zinaelekea kufungua ukurasa mpya wa historia ya uhusiano kati ya nchi hizo mbili.

Bwana Macron anatarajiwa kutembelea na kutoa hotuba kwenye kumbukumbu ya mauaji ya kimbari ya Kigali. Anatarajiwa pia kumteua balozi Ufaransa mjini Kigali - ambaye atakuwa wa kwanza katika kipindi cha miaka sita.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...