Washington,Rais Joe Biden wa Marekani ametoa wito wa kusitishwa mapigano kati ya Israel na wanamgambo wa Hamas, wenye kulitawala eneo la Gaza, katika mazungumzo yake ya njia ya simu na Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu.Taarifa ya Biden imetolewa kwa uangalifu mkubwa, ikitajwa kuwa ni rai ya awamu ya pili kutolewa na Ikulu ya Marekani, kufuatia shinikizo kubwa katika kipindi ambacho mashambulizi yakiendelea.K
iongozi huyo wa Marekani ameitaka Israel pia kufanya kila linalowezekana kuwanusuru raia wasio na hatia.
Awali Jumatatu Waziri Mkuu Netanyahu aliviambia vikosi vya usalama kwamba Israel itaendelea na mapambano hayo ambayo yamedumu kwa takribani siku 8 na kusababisha zaidi ya watu 200 kufariki dunia wengi wao wakiwa Wapalestina.

No comments:
Post a Comment