Indonesia imeachilia meli ya mafuta ya Iran, ambayo iliikamata mnamo Januari 24, kwa tuhuma za kubeba mafuta ya magendo.
Kulingana na taarifa ya shirika rasmi la Iran la IRNA, ambalo linahusiana na Kampuni ya Kitaifa ya Tanker ya Iran, ilielezwa kuwa kutokana na juhudi za kidiplomasia, meli ya mafuta iliyokuwa na bendera ya Iran "MT Horse" ilianza tena msafara wake hapo jana jioni.
Meli hiyo ya mafuta itarudi Iran baada ya kumaliza shughuli yake msafara.
Mnamo Januari 24, Indonesia ilinakamata meli mbili zilizokuwa na bendera ya Iran na Panama zinazoshukiwa kubeba mafuta ya magendo, na kuwazuia Wairani 36 na Wachina 25 waliokuwa wakifanya kazi kwenye meli hizo.

No comments:
Post a Comment