Search This Blog

Saturday, May 22, 2021

Mafuriko nchini Malaysia


Takriban watu elfu 5 wamehamishwa kutoka katika nyumba zao kwa sababu ya mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa katika majimbo ya Sabah na Sarawak nchini Malaysia.


Kamati ya Usimamizi wa Maafa ya Sabah imetangaza kwamba idadi ya raia waliohamishwa baada ya mvua ambazo zimekuwa zikinyesha katika jimbo kwa siku 3 zilizopita imeongezeka hadi 4,772.


Kamati ya Usimamizi wa Maafa ya Sarawak imetangaza kuwa watu 326 wamehamia maeneo salama kwa sababu ya mafuriko.


Wakibainisha kwamba mvua itaendelea, maafisa hao wamesema kwamba idadi ya maeneo salama itaongezwa katika majimbo yote mawili.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...