Takriban watu elfu 5 wamehamishwa kutoka katika nyumba zao kwa sababu ya mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa katika majimbo ya Sabah na Sarawak nchini Malaysia.
Kamati ya Usimamizi wa Maafa ya Sabah imetangaza kwamba idadi ya raia waliohamishwa baada ya mvua ambazo zimekuwa zikinyesha katika jimbo kwa siku 3 zilizopita imeongezeka hadi 4,772.
Kamati ya Usimamizi wa Maafa ya Sarawak imetangaza kuwa watu 326 wamehamia maeneo salama kwa sababu ya mafuriko.
Wakibainisha kwamba mvua itaendelea, maafisa hao wamesema kwamba idadi ya maeneo salama itaongezwa katika majimbo yote mawili.

No comments:
Post a Comment