Search This Blog

Tuesday, May 25, 2021

Maduro atoa wito wa kufunguliwa kwa pande zote za mipaka kati ya Colombia na Venezuela


Rais wa Venezuela Nicolas Maduro alitaka kufunguliwa kwa pande zote za mipaka na Colombia, ambayo imefungwa tangu Februari 2019.

Akifahamisha kuwa alitaka kuratibu "ufunguliwaji wa milango tena" kwa mipaka yao na Colombia, Maduro alisema,

"Kwa kweli inawezekana kufungua mipaka ya udhibiti. Colombia inazungumza juu ya kufunguliwa mipaka bila upande mmoja pekee. Ninawaambia kufungua kwa upande mmoja pekee hakusaidii chochote."

Katika taarifa iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Colombia, ilielezwa kuwa uwezekano wa kufungua tena mipaka na Venezuela kwa kuchukua hatua maalum ulijadiliwa mnamo Juni 1 kama sehemu ya kufufua shughuli za kiuchumi.

Uhusiano kati ya nchi hizo mbili ulivurugika baada ya serikali ya Rais wa Colombia Ivan Duque kumtambua Rais wa Bunge la wakati huo Juan Guaido, ambaye alijitangaza kuwa rais nchini Venezuela mnamo Januari 23, 2019, kama "rais halali".

Katika taarifa yake mnamo Februari 23, 2019, serikali ya Venezuela iliamua kufunga mipaka na Colombia kwa muda, ikitaja "vitisho vikali na ukiukaji."

Maduro aliwaambia waandishi wa habari mnamo Februari 24, 2019 kwamba walikuwa wamekata uhusiano wa kidiplomasia na Colombia na walimpa Balozi wa Colombia masaa 24 kuondoka Venezuela.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...