Search This Blog

Saturday, May 8, 2021

Kundi watu wenye silaha lateka nyara wanafunzi wa chuo kikuu nchini Nigeria

 


Idadi kubwa ya wanafunzi wa chuo kikuu walitekwa nyara kwenye shambulizi la watu wenye silaha lililoendeshwa katika jimbo la Abia nchini Nigeria.

Kamishna wa Habari wa Jimbo la Abia John Kalu, alisema watu wenye silaha walishambulia gari lililokuwa limebeba wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Jimbo la Abia (ABSU) kwenye barabara kuu ya jimbo la Okigwe-Uturu.

Kalu alisema kuwa wanafunzi wengi walitekwa nyara katika shambulizi hilo ambapo wanafunzi wengine 2 walifanikiwa kutoroka.

Akibainisha kwamba walishirikiana na vikosi vya usalama katika jimbo jirani la Imo kuwaokoa wanafunzi waliotekwa nyara, Kalu alisema,

"Tunapendekeza umma na jamii ya ABSU ibaki na utulivu kwa sababu hatutatenga rasilimali yoyote kuhakikisha usalama wa wahanga."

Katika majimbo ya Nigeria kama Benue, Plateau, Katsina na Zamfara, shule zilishambuliwa mara kadhaa tangu Januari na wanafunzi walitekwa nyara.

Wanafunzi 16 walitekwa nyara katika shambulizi la watu wenye silaha lililotekelezwa mnamo Aprili 20 kwenye Chuo Kikuu cha Kibinafsi cha Green Field katika jimbo la Kaduna.

Shughuli za masomo zilisitishwa katika baadhi ya majimbo kwa sababu ya mashambulizi yaliyolenga shule nchini Nigeria.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...