Search This Blog

Wednesday, May 19, 2021

Kuna tatizo kwenye kununua LUKU- TANESCO


Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limeomba radhi wateja wake kutokana na hitilafu iliyotokea kwenye Mfumo wa Manunuzi ya Umeme wa LUKU.

Hitilafu hiyo imetokea kuanzia Mei 17, 2021 na kusababisha baadhi ya wateja kushindwa kununua umeme.

TANESCO imeomba uvumilivu kwa muda huu ambao tatizo linaendelea kutatuliwa.

“Tunawaomba radhi kutokana na hitilafu iliyotokea kwenye mfumo wa manunuzi ya umeme wa LUKU siku ya Jumatatu, Mei 17, 2021 na kusababisha baadhi ya wateja kushindwa kununua umeme. Tunaomba uvumilivu wakati wataalamu wetu wanafanya kazi kuhakikisha tatizo hilo linatatuliwa haraka” TANESCO 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...