Search This Blog

Thursday, May 20, 2021

Kim azuia matumizi ya dawa na chanjo za China


Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un alipiga marufuku utumiaji wa dawa na chanjo za China katika hospitali za mji mkuu wa Pyongyang.

Kulingana na taarifa za Asia News, kutokana na kufariki kwa afisa mwandamizi wa Korea Kaskazini baada ya kutumia dawa inayotengenezwa na China, kiongozi wa nchi hiyo Kim Jong-un alizuia matumizi ya dawa na chanjo dhidi zinazozalishwa China dhidi ya corona (Covid-19) katika hospitali za mji mkuu wa Pyongyang.

Hata hivyo, bado haijathibitishwa wazi iwapo dawa aliyotumia afisa mwandamizi ilisababisha kifo chake.

Wakati maafisa wa Korea Kaskazini wanadai kuwa hakuna kesi za Covid-19 nchini humo, ukweli wa madai hayo unahojiwa na mashirika ya kimataifa na jumuiya ya wanasayansi.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...