Japan ilitangaza kuwa inaweza kusimamisha misaada yake rasmi ya maendeleo kwa Myanmar, ambayo ilikumbwa na mapinduzi mnamo Februari na kuendeshwa kwa utawala wa jeshi.
Katika mkutano na waandishi wa habari, Waziri wa Mambo ya Nje Motegi Toshimitsu alisema kuwa watu wa Myanmar na jamii ya kimataifa wanatarajia kubadilisha mwelekeo huo.
Akifahamisha kuwa ikiwa hakuna mabadiliko katika hali ya kijamii nchini Myanmar, nchi yake inaweza kusitisha misaada ya maendeleo inayotolewa kwa Myanmar, Motegi alisema kuwa serikali ya Japan inafuata juhudi zinazofanywa na Chama cha Mataifa ya Kusini Mashariki mwa Asia (ASEAN) kubadili hali hiyo.
Shirika la utangazaji wa umma NHK lilikumbusha kwamba Japan hapo awali iliamua kutosaini mikataba mipya ya misaada ya maendeleo, na kwamba misaada kamili iliyosainiwa bado inaendelea.

No comments:
Post a Comment