Search This Blog

Friday, May 7, 2021

China yapuuza kitisho cha madhara ya roketi inayotarajiwa kuanguka duniani

 


China imepuuza kitisho cha madhara yanayoweza kusababishwa na roketi iliyoanguka kutoka kwenye mzingo wa dunia baada ya kujiachanisha na kituo cha masuala ya anga cha China baada ya Marekani kuonya huenda ikaanguka kwenye eneo la makazi ya watu duniani. 

Wataalamu wa kijeshi nchini Marekani wanataraji kwamba roketi hiyo aina ya Long March 5B itaanguka duniani kati ya Jumamosi na Jumapili, lakini wakionya ilikuwa ni vigumu kukisia itaangukia wapi na wakati gani hasa. 

Hata hivyo msemaji wa wizara ya mambo ya kigeni wa China Wang Wenbin amesema uwezekano wa kusababisha madhara ni mdogo mno. 

Amesema kwa kiasi kikubwa roketi hiyo itaharibika itakapokuwa ikianguka na kwamba mamlaka zitauarifu umma juu ya hali ilivyo katika wakati unaofaa.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...