Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani Anthony Blinken atazuru Israel na mamlaka ya Palestina kwenye eneo linalokaliwa kimabavu la Ukingo wa Magharibi.
Chanzo kilichoarifu kuhusiana na ziara hiyo kimesema Blinken atazuru maeneo hayo siku ya Jumatano na Alhamisi kama sehemu ya juhudi za Washington za kuimarisha makubaliano ya Gaza.
Maafisa wa Marekani, Israeli na Palestina hata hivyo bado hawajachapisha ratiba ya ziara hiyo ya Blinken, lakini wizara ya mambo ya kigeni ya Marekani ilitangaza ziara hiyo siku ya Alhamisi ikisema atazungumzia juhudi za kusaidia kuanza upya na kushirikiana kujenga mustakabali bora kwa Israel na Palestina.
Rais Biden tayari ameahidi kuisaidia Gaza kujijenga upya. Blinken pia atazuru Misri iliyosimamia makubaliano ya Gaza ya kusitisha mapigano kati ya mataifa hayo mawili pamoja na Jordan.

No comments:
Post a Comment