Search This Blog

Sunday, May 16, 2021

Baraza la Usalama kukutana kwa ajili ya mapigano ya Gaza

 


Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linakutana leo Jumapili, baada ya mashambulizi ya Israel katika ukanda wa Gaza kuwaua watoto 8 na kuharibu majengo yaliyokuwa na ofisi za vyombo vya habari. 

Hapo jana vikosi vya Israel viliushambulia ukanda wa Gaza, ikiwa ni siku ya sita ya urushaji mabomu katika eneo hilo la Palestina linalodhibitiwa na kundi la Kiislamu la Hamas ambalo nalo lilijibu kwa kufyatua maroketi. 

Wakati Baraza la Usalama likijiandaa kukutana, jeshi la Israel limesema hii leo kuwa limeyalenga makaazi ya kiongozi wa juu wa kundi la Hamas. 

Msemaji wa jeshi la Israel Brigedia Jenerali Hidai Zilberman amesema jeshi liliyalenga makaazi ya Yehiyeh Sinwar kiongozi mwandamizi wa Hamas katika eneo hilo na kuna uwezekano amejificha pamoja na wanachama wengine waandamizi. 

Hamas imekiri kuwa wapiganaji wake 20 wameuawa tangu mapigano yaanze.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...