AZAM FC inaayonolewa na Kocha Mkuu, George Lwandamina leo Aprili 25 imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Azam FC katika mchezo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa Uwanja wa Mkapa.
Kipindi cha kwanza timu zote zilitoshana nguvu na kuwafanya waende vyumba vya kubadilishia nguo ubao ukisoma Yanga 0-0 Azam FC.
Ni Prince Dube dakika ya 85 alipachika bao la ushindi nje ya 18 na kumfanya afikishe jumla ya mabao 12 akiwa ni kinara kwa utupiaji ndani ya Ligi Kuu Bara.
Ushindi huu unaifanya Azam FC kulipa kisasi cha kupoteza mchezo wao uliopita ambapo walifungwa bao 1-0.
Kwenye msimamo Azam FC baada ya kucheza mechi 28 inafikisha jumla ya pointi 54 ikiwa nafasi ya tatu huku Yanga ikiwa na pointi 57 baada ya kucheza mechi 27 nafasi ya pili na kinara wa ligi ni Simba mwenye pointi 58 baada ya kucheza mechi 24.

No comments:
Post a Comment